Msanii wa muziki wa kiazi kipya anayejulikana kama
Diamond Platnumz hivi karibuni alilazimika
kuahirisha ziara yake ya barani Ulaya baada ya waandaaji kushindwa kukamilisha malipo
yake ya advance katika muda unatakiwa kutokana mna makubaliano.
Kwa habari zilizokuwepo ni kuwa Diamond alitakiwa kulipwa
50,000 USD (Dollar) ambazo ni sawa na shilingi 80 Million za Kitanzania.
Diamond alizidi kufunga kuwa ziara hiyo itafanyika mwezi
ujao ambapo baada ya ziara hiyo atarudi nyumbani Tanzania na kisha kujiandaa tena kwaajili ya ziara nyingine.
Kutokana na makubaliano mapya ya ziara hiyo kuna
uwezekano wa ziara hiyo ya kwanza kumuingizia karibu shilingi milioni 100 ama
zaidi.
Jumamosi hii Diamond alilazimika kutumia website yake
kutoa taarifa ya kuahirisha kwa ziara hiyo.
“Kutokana na kampuni ya United Events Ltd Tilburg-The
Netherlands kwa upande mwingine kama promoter kushindwa kutimiza baadhi ya
mahitaji ikiwemo kushindwa kulipa pesa ya show ambayo ilitakiwa ifanyike
Jugenhause Ostend mjini Stuttgart/Germany 09/03/2013 na zingine kama East
African Night ambayo ilitakiwa ifanyike mjini Rotterdam/Holland tarehe
15/03/2013 na kadhalika, mimi na team yangu nzima ya wasafi hatutoweza
kuhudhuria kwenye events hizo,” alisema.
“Nilikuwa nikipata maswali mengi sana toka kwa mashabiki
zangu mbalimbali wakiniuliza kuhusiana na ujio wangu wa nchi hizo za EUROPE
lakini siku zote nilikua kimya sikuweza kujibu wala kuzungumza chochote na
wadau wangu kutokana na kutokuwa na uhakika wa tour hiyo.”
Post a Comment