Mimi ni mama wa miaka 36, nina watoto watatu, nina miaka tisa kwenye ndoa, tulipoona na mume wangu tulikuwa tukifanya mapenzi style za kawaida tu, tunabadili style lakini ni zile za kawaida

Umefika miezi mwala sasa mume wangu amebadilika sana, yani hatulii yani mimi nayeye hatukai nusu saa bila ugomvi, kitu kidogo tu, hasira kwangu na anapeleka hadi kwa watoto wangu, yani hadi wanamuogopa sasa hivi, wakimuona tu! Wote wanaenda kulala,



Hadi sasa nahisi mume wangu anamwanamke nje, tena ni Malaya kabisa, maana violet mdogo wangu, mume huyu huwa nakaa namfikiria naona kama wamenirogea vile, hajui kubembeleza kwenye mapenzi, yeye ni kuamrisha tu, tofauti na zamani, hata mimi nikimbembeleza labda nimshike shike sehemu ambazo najua akishikwa anafurahi, nimnyonyenyonye hapa na pale, zamani alikuwa anapenda sana. Siku hizi hataki kabisa, nikianza tu, anasema ah! Nimechoka mimi, kwanza nimeshaoga unanipaka matemate yako, wakati bafu liko hapo chumbani angeweza kuoga tena,



Sasa kuna kipindi nami niliamua kukaa kimya, nikawa nasubiri hadi yeye aanze, lakini sasa style alizokujanazo sasahivi mimi siziwezi, yani sio za kawaida, nina mwili mkubwa, nilizaa kwa operation, nina kovu tumboni, siwezi kujikunja kunja Napata maumivu, sasa yeye utakuta ananikunja kama samaki, yani nabanwa nakuwa mdogo, nalia sana, sio kwa raha ila ni kwamaumivu, na hata nikilia anasema nisubiri hadi amalize ndio aniache, akiniacha tu! Ujuwe lazima nitalala hata siku mbili, naumwa sana kiuno,


Kuna siku nilimuuliza kwanini ananifanya kama ananibaka vile, akasema akifanya style za zamani hasikii raha kabisa, kuna kipindi alianza kuniambia kuwa anataka anifanya nyuma, sikuamini masikio yangu, nililia sana, nikamwambia ndoa na ife, narudi kwetu, akanisihi nibaki, nashukuru hakurudia tena kutamaka ushenzi huo,


Style zake za sasa hivi sijui anazitoa wapi, yani sasahivi akiniambia kama anahitaji tu! Basi naweza meza hata dawa ili nijifanye naumwa, napoteza furaha kabisa, yani hawezi kabisa kunifanya kawaida, naombeni mnishauri nifanyaje, maana ni kweli kwa mwanamke yeyote Yule style ninazofanywa mimi, lazima angelia, mimi hadi huwa nakwenda hospitali, ila nikifika sisemi kama nimefanya style mbaya, huwa nadanganya maana naona ni aibu, nitamuaibisha mume wangu na mimi pia.

Post a Comment

 
Top