Rapper Rick Ross ameshare picha ya msanii wake Meek Mill akiwa jela. Taarifa zinasema mpaka sasa mahakama haijasema ni muda gani Meek Mill atakaa jela. Mmiliki wa Maybach Music Group Rozay ameweka picha ya rapper wake akiwa jela kuwajulisha mashabiki wake kuwa Meek yupo salama na ana afya nzuri tu.
Meek_Prison
Meek Mill yupo jela kwa kosa la kuvunja amri alizopewa na mahakama wakati akiwa kwenye kifungo cha nje ambapo alijihusisha na biashara ya dawa za kulevya mwaka 2009 na kukutwa na silaha kinyume cha sheria. Mwezi wa saba alihukumiwa kurudi jela kwa miezi sita na kukataliwa kutoka mapema kwa kigezo chochote.
Meek_Prison 2

Post a Comment

 
Top