Mwenyekiti Kiongozi wa Chama cha ACT - Wazalendo, Zitto Kabwe ametoa yake ya Moyoni kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani,Mh Edward Lowassakuwa kama anataka kugombea urais kupitia cha ACT basi afuate mashati yote ikiwa ni pamoja na kutangaza mali zake anazomiliki ikiwa ni sheria ndani ya chama hicho.


zitto kabwe
 
Gazeti lako la Mwanzanichi limeandika kama ifuatavyo

Akiwahutubia mamia ya wakazi wa Jiji la Mwanza kwenye Viwanja vya Furahisha juzi, Zitto alisema hawezi kumzuia mtu anayetaka kujiunga ACT - Wazalendo ikiwa atafuata taratibu zilizowekwa na chama hicho.


“Naomba niwaambie Watanzania kwamba ACT siyo chama cha kumtengenezea mtu mazingira ili agombee urais, lakini kama Lowassa anataka kugombea urais kupitia huku lazima atangaze mali zake na kueleza wapi amezipata kama taratibu za chama zinavyosema,” alisema Zitto na kuongeza:


Zimekuwapo taarifa kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuwa baadhi ya wagombea akiwamo Lowassa ambaye anatajwa kuwania urais kupitia CCM, wana mpango wa kutimkia ACT iwapo watakatwa majina yao katika mchujo wa wagombea.


Kwa mujibu wa habari hizo, ACT - Wazalendo imepewa fedha na Lowassa ambazo inatumia katika mikutano hiyo kumwandalia nafasi ya kuwania urais, madai ambayo pande zote zimeyakanusha.


Akizungumzia taarifa hizo kwenye mkutano huo, Zitto alisema chama chake kinaongozwa kwa kufuata taratibu na kitampokea yeyote atakayefuata taratibu hizo.


Kiongozi huyo ambaye hivi karibuni alitangaza mali na madeni yake, alisema iwapo Lowassa atataka kujiunga na chama hicho itambidi atangaze mali zake na kueleza jinsi alivyozipata, kama yeye (Zitto) alivyofanya.


Hata hivyo, akizungumzia kuhusu kauli ya Zitto, msemaji wa Lowassa, Aboubakary Liongo alisema: “Hakipo kitu kama hicho na hakitakuwapo, hatujui habari hii inatoka wapi? Mzee (Lowassa) amekuwa akitumikia CCM maisha yake yote tangu enzi za TANU … yupo na anaendelea kutumikia kifungo chake. Maisha yake yote ni mtumishi wa chama.”


Lowassa pamoja na makada wengine watano wa chama hicho walipewa adhabu ya onyo kali baada ya Kamati Kuu ya CCM kuwatia hatiani kwa kuanza kampeni za urais mapema na kukiuka maadili ya chama.


Mbali ya Lowassa, wengine waliofungiwa ni Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye; Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja; Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira; Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe; na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba.


Licha ya muda wa adhabu hiyo kufikia tamati tangu Februari mwaka huu, chama hicho kilisema kinaendelea kuchunguza mienendo yao na hakijaeleza hatma yao.


Juzi, gazeti hili liliripoti kuwapo kwa mkakati wa chama hicho kukata majina ya baadhi ya wagombea wanaoaminika kuwa na makundi yanayokihatarisha, wakilengwa Lowassa na Membe ili kipitishe mgombea asiyekuwa na kundi.

Post a Comment

 
Top