diamond platnumz

Diamond Platnumz kwa mara nyingine amepata nafasi ya kuiwakilisha Tanzania kwenye tuzo kubwa za kimataifaa. 

Ametangazwa kuwania tuzo za MTV Europe Music Awards 2015 (MTV EMA) katika kipengele cha Best African Act.


Wasanii wengine wa Afrika ambao atachuana nao kwenye kipengele hicho ni AKA (South Africa), Yemi Alade (Nigeria), Davido (Nigeria).


Hata hivyo bado anatafutwa msanii mmoja kukamilisha idadi ya nominees watano katika kipengele hicho, ambaye atapatikana kwa kura za mashabiki kupitia Twitter. 

Wasanii ambao wametajwa na MTV wapigiwe kura ili apatikane mmoja ni Wizkid (Nigeria), K.O (South Africa), Stonebwoy (Ghana), Cassper Nyovest (South Africa) pamoja na Dj Arafat (Côte d’Ivoire). Kura zinapokelewa hadi September 14 saa 23:59


2015 MTV EMAs zitafanyika Octoba 25, 2015 jijini Milan, Italy ikiwa ni mara ya tatu kufanyika nchini humo na mara ya pili kufanyika kwenye jiji la Milan.

Post a Comment

 
Top