Home
»
SIASA
» Aliyekuwa Mgombea wa Ubunge Kinondoni ACT Kalapina Kuibuka Mahakamani Kupinga Matokeo.
Aliyekuwa Mgombea Mbunge katika Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya Chama cha ACT-Wazalendo, Kalama Masoud ‘Kalapina’ ameibuka na kupinga matokeo akidai atakwenda mahakamani.
Akizungumza na wanahabari leo Makao Makuu ya chama hicho Kijitonyama jijini Dar es Salaam, Kalapina amesema matokeo yaliyompa ushindi mgombea wa chama cha wananchi CUF ambaye alikuwa anaungwa mkono na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA, Abdul Mtulia yalikuwa yamesheheni dosari kubwa.
Amesema katika kata 19 zilizopo katika Jimbo la Kinondoni, mawakala wake walitishiwa na kulazimika kuacha kusimamia vituo walivyokuwa wamepangiwa.Kalapina alitaja baadhi ya maeneo aliyodai mawakala wake walitishiwa na baadae kuamua kuondoka kuwa ni kata za kijitonyama,Tandale, Ndugumbi pamoja na Kigogo.
Alieleza kuwa baada ya kubaini matatizo yote hayo alilazimika kugomea kusaini karatasi ya wagombea ubunge, akiongeza kuwa hatua iliyobaki kwa sasa ni kwenda kufungua kesi mahakamani.“Natarajia kwenda mahakamani kutaka haki, kwa hiyo Jumatatu au Jumanne ijayo nakwenda kufungua kesi,” alisema kalapina.
Related Posts
- Chama Cha Mawakala wa Forodha Nchini Chaibua Mapya Kuhusu Utoroshwaji wa Makontena15 Dec 20150
CHAMA cha Mawakala wa Forodha nchini (TAFFA) kimesema kuwa wizi wa kontena bandari ya Dar es ...Read more »
- David Kafulia Kunguruma Mahakama Kuu Kupinga Ushindi wa CCM Jimbo la Kigoma Kusini.17 Nov 20150
Aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini kupitia chama cha NCCR -Mageuzi, David Kaful...Read more »
- CCM Yazoa Viti Maalum Vya Udiwani 1021 Huku Wapizani Wachukua Viti 371 Tu.14 Nov 20150
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), imetangaza idadi ya viti maalum kwa nafasi ya udiwani ...Read more »
- Picha za Maalim Seif Pamoja na Viongozi wa Ukawa Wakizungumza na Balozi wa EU na Kutoa Msimamo Mzito.14 Nov 20150
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, amerejea kauli yake ya k...Read more »
- Nape Nnauye Aelezea Sababu za Jina la Irene Uwoya Kukatwa kwenye Ubunge wa Viti Maalum.10 Nov 20150
Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),Nape Nnauye amefunguka suala la msanii wa Bong...Read more »
- Wagomba Zanzibar Waandika Barua Umoja wa Mataifa UN.04 Nov 20150
Wagombea wa urais wa Zanzibar wa vyama sita, wamemwandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mata...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.