Kundi la muziki nchini Kenya linalofanya vizuri
sana Africa Mashariki linalojulikana kama Sauti Sol linatarajia kusafiri kuelekea jijini
Lagos nchini Nigeria kuipeperusha bendera ya taifa la Kenya katika tamasha linalojulikana kama Inaugral
Viewers’ Choice Awards litakalofanyika jumamosi hii nchini Nigeria.
Sherehe hizo zitasindiikizwa na magwiji wa muziki barani
Afrika kama Femi Kuti, Tiwa Savage,
Chidinma na wengineo wengi.
Aidha Sauti Sol watapata nafasi ya kujumuika na nyota
wengine wa filamu nchini Nigeria kama vile Chinedu Ikedieze, Genevieve Nnaji,
Majid Michel, Omotola Jalade-Ekeinde, Rita Dominic na wengineo kibao watakokuwa
wakishiriki katika utoaji wa tuzo hizo
Post a Comment