Waandishi wa habari wakifuatilia hotuba ya Waziri Nchimbi.
Makamanda wa vikosi mbalimbali wakisikiliza hotuba ya waziri.
Baadhi ya askari wa JKT waliohusika katika zoezi la uokoaji.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Sera), William Lukuvi, akitoka eneo la tukio mara baada ya Dk. Nchimbi kuhutubia.
Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji, Kamishna Jenerali, Nyambacha (kulia) akitoka eneo la tukio na makamanda wengine.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, DCP Suleiman Kova, akitoka eneo la tukio, kushoto kwake ni mwandishi wa habari akimdodosa jambo.
Shimo ambalo ghorofa lilijengwa, hapa ni baada ya kifusi chote kuzolewa.
Baadhi ya waokoaji wa Kichina.
Makamanda wa JWTZ wakijadiliana mara baada ya kazi kuisha.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, ACP Marieta Minagi (kulia) akiwa eneo hilo.
Askari wa kikosi cha usalama barabarani wakiondoka eneo la tukio.
 ILE operesheni ya kufukua kifusi cha ghorofa iliyoanguka jijini Dar es Salaam imehitimishwa leo na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi. Jumla ya maiti 34 zimepatikana na watu waliojeruhiwa na kuokolewa wakiwa hai ni 18.
 (PICHA: Haruni Sanchawa na Gladyness Mallya)

Post a Comment

 
Top