Msanii Hussein Ramathan Mkeit almaruufu kama Sharo millinea jana usiku baada ya kupata ajali ya gari iliyotokea mida ya saa mbili usiku maeneo ya Muguzoni songa katikati ya Segera na mkoani Tanga

Habari hizi zimedhibitishwa na kamanda wa polisi mkoani Tanga Constatine Massawe.Kwamujibu wa kamanda huyo,gari aina ya Toyota Harrier lenye namba za usajili T 478 BBR alilokuwa akiendesha yeye mwenyewe lilipo fika eneo hilo lilacha njia na kuelekea pembeni hivyo kupinduka ambapo ilisababisha umauti wake,inasemeka marehemu alikuwa akitokea Dar es salaam kulekea muheza.Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospital taule ya Muheza

Kishymba.blogspot.com inaungana watanzania wote katika msiba wa mwenzetu
MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAALI PEMA PEPONI AMEEN

Post a Comment

 
Top