Katika hali isiyo kuwa ya kawaida msanii wa filamu na muziki Bongo, Baby Joseph Madaha hivi karibuni alinaswa nyumbani kwa kigogo anayetoka na Wema anayejulikana kwa jina Clement.

Kwa mujibu wa chanzo kilichoomba hifadhi ya jina lake, tukio hilo lilitokea hivi karibuni ambapo staa huyo wa filamu na muziki alionekana akiingia kwa usafiri wa teksi nyumbani kwa kigogo huyo anayeishi maeneo ya Mwananyamala-Gereji, Dar.

Baada ya kujiridhisha na maelezo ya sosi huyo, mapaparazi wetu walimtafuta Baby Madaha ili kujua ukweli wa jambo hilo.

“Kweli nilikwenda hapo (kwa Clement), mimi sijui kama niliyeenda kuonana naye ni bwana wa Wema kwa sababu sijawahi  kumuona naye na nilimfuata kwa ajili ya kuzungumza mambo ya kikazi,” alisema Baby Madaha.

Source Global publisher

Post a Comment

 
Top