Wananchi  wakiwa  wamenyosha  mikono  juu  kuunga mkono hatua ya  mbunge Msigwa na  Chama cha Chadema  kuja na  wazo la kupinga kodi katika line za simu
 Wananchi wakiwa  wametulia  kusikiliza maneno matamu ya mbunge Msigwa
 Mbunge Msigwa  akisikiliza  swali kutoka kwa mwananchi
 Mbunge Msigwa  akimbembeleza  mwananchi  kuulizwa  swali baada ya kupanda  jukwaani na kushindwa kuuliza swali kwa madai  kuwa  swali lake  limepotea njiani  wakati akipanda  jukwaani kutokana kuona aibu  umati mkubwa wa  wananchi

 Mkazi  wa Iringa Maneno Mbuma akiuliza swali kwa mbunge 
 Mheshimiwa mimia  sina swali naomba  kuomba ridhaa ya  wananchi  kuonana na  wewe faragha ili  tuongee faragha
 Wakazi  wa Kihesa  waliofika katika mkutano  huo








 Uchangiaji  wa ujenzi wa ofisi ya kata ya  Chadema
MBUNGE  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji  Peter Msigwa ( Chadema) amewataka  wananchi  wa  jimbo la Iringa mjini  kujiandaa kujaza  fomu maalum  za kupinga uamuzi wa  serikali ya  CCM chini ya  waziri wa  fedha Dr Wiliam Mgimwa kutaka wamiliki  wa  simu kuanza  kulipia kodi ya  Tsh 1000 kwa  kila kadi (line) ya  simu .

Mbunge  Msigwa  ametoa wito  huo  leo katika  mkutano  wa hadhara  uliofanyika katika  viwanja  wa ofisi ya kata ya Kihesa mjini hapa.

Alisema  kuwa Chadema hakipotayari  kuona  serikali  ya  CCM ikiendelea kuwakandamiza  wananchi  wanyonge  kwa  kuwawekea  kodi katika line  zao  za simu jambo ambalo alisema  ni mzigo kwa  mtanzania na  kuwa kamwe  suala hilo  watalipinga kwa nguvu  zote na kuomba wananchi  kujiandaa kujaza fomu maalum ambazo  zitaanza  kupitishwa katika  mikutano yake  itakayoanza  hivi karibuni .

Mbunge Msigwa  alisema tayari  zoezo kama  hilo amelianza mbunge wa  jimbo la Ubungo John Mnyika  na kuwataka  wananchi  wa Iringa  kujitokeza kwa  wingi katika mikutano yake ambayo itakwenda sambamba na  kupinga  uamuzi huo kandamizi  wa serikali  wa  kutoza kodi katika line za simu.

" Nawaombeni mara  baada ya  kuanza  zoezi hilo  la  kujaza  fomu  kila mmoja ashiriki kwa kujaza jina lake na namba  yake ya  simu ili kupeleka fomu  hizo  bungeni kupinga  uamuzi  huo ambao umepitishwa na  wabunge wa CCM "

Post a Comment

 
Top