Al Sisi alitazamiwa kujiuzulu na anatarajiwa kushinda kwa ukubwa.
Mkuu wa majeshi na waziri wa
ulinzi Misri, Abdul Fattah al-Sisi, ametangaza kujiuzulu jeshini ili
kugombea katika uchaguzi wa urais mwezi ujao.
Ni Bayana kwana Sisi hatakua na kibarua kigumu
kujipatia ushindi katika uchaguzi wa Urais. Anaungwa mkono na idadi
kubwa ya raia wa Misri na hadi sasa hana wapinzani wowote.
Baadhi ya waliotaka kugombea urais wamejiondoa wakidai kwamba hawataweza kuendesha kampeni zao kwa njia huru.Wafuasi wake Sisi wanamuona kama kiongozi imara ambaye anaweza kurejesha amani na udhabiti nchini Misri baada ya miaka mingi ya machafuko.
Wakosoaji wake wanasema ana msimamo mkali na amechangia pakubwa katika kusambaratisha na kuhujumu upinzani nchini Misri.
>>>>>Na bbcswahili
Post a Comment