Mwanafunzi mmoja alikuwa amekaa kwenye daladala anaandika sms,huku ameshika begi lake.
Mzee mmoja wa kiswahili kando yake akaanza kuangalia dogo anaandika nini.
 
Dogo alipogundua anachunguliwa akaamua kubadilisha sms akaanza kuandika:
 
"Yule nyoka uliyenipa inakaa hujamtoa meno ya sumu,hapa nilipo anasumbua kwenye begi anataka kutoka,sijui nifanyeje na alivyo mkubwa akitoka ataleta taabu coz niko ndani ya matatu."...
Mzee kuona vile akaanza kusogea pembeni.
Dogo alipoona mzee anababaika akachukua begi na kumrushia...Mzee akaruka dirishani fasta huku akipiga kelele,"Mamaae nyokaaaaa!....nakufa mieee!

Post a Comment

 
Top