bibi harusi aliyetoka siku ya harusi yako moshi apatikana

Bibi harusi Doroth Msuya aliyetoroka saluni

akipambwa saa tatu kabla ya kufungwa kwa harusi

yao na kumwacha solemba bwana harusi, Joseph

Machange amepatikana jijini Arusha.

Polisi mkoani Kilimanjaro imesema binti huyo

hakutekwa nyara kama ambavyo wanafamilia

walitoa taarifa Kituo cha Polisi Himo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Fulgence

Ngonyani alisema jana kuwa uchunguzi uliofanywa

umethibitisha kuwa bibi harusi huyo hakuwa

ametekwa nyara.

“Polisi walifungua jalada la uchunguzi na ilibainika

kuwa taarifa za kutekwa zilizokuwa zimetolewa

hazikuwa na ukweli, bali aliondoka kwa kupanda

pikipiki,” alisema.

Kamanda Ngonyani alisema uchunguzi huo ulibaini

kuwa wakati akipambwa, aliomba kwenda

kujisaidia na baadaye kuomba apelekewe kanga na

‘tishu’ lakini akatumia mwanya huo kuondoka,”

alisema.

Alisema uchunguzi huo umebaini kuwa baada ya

kupanda pikipiki ilimpeleka hadi kituo cha mabasi

na alimlipa dereva wa bodaboda kisha alipanda

gari la abiria lililompeleka hadi mjini Moshi.

Tukio hilo lilitokea Jumamosi iliyopita saa 6.30

mchana eneo la Lole huko Mwika, Moshi wakati

bibi harusi huyo alipotoroka saluni akimwacha

mpambe wake akiendelea kupambwa.

Ndoa hiyo ilikuwa ifungwe saa tisa alasiri katika

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT),

Usharika wa Lole Dayosisi ya Kaskazini na baadaye

sherehe ingefanyika katika Ukumbi wa Mamba

Complex.

Habari zilizopatikana jana kutoka kwa familia ya

Machange, zilieleza kuwa Doroth alipatikana juzi

baada ya kuonekana akiweweseka, kisha

akapelekwa hospitali ya Seliani kwa matibabu.

Ndugu wa karibu wa familia ya Machange ambaye

aliomba jina lake lisitajwe, alisema kulikuwa na

kikao kilichokuwa kikiendelea kati ya familia ya

Machange na Msuya.

“Jana (juzi) tulipigiwa simu na kuelezwa kuwa

Doroth amepatikana Arusha lakini yuko kama

hajielewielewi na hajui nini kimetokea,” alisema.

Habari zaidi kutoka ndani ya familia hiyo, zinadai

kuwa bibi harusi huyo alikuwa ametaka harusi hiyo

iahirishwe na ombi hilo alilitoa zaidi ya mara 10

bila kueleza sababu.

Source:Mwanachi

Post a Comment

 
Top