Taarifa ambayo kila aliekua karibu na Goldie kwenye page zake za facebook na twitter inakua ngumu kuamini, taarifa rasmi zimeripoti kwamba Goldie ambae ni mwakilishi wa Nigeria kwenye BBA 2012 AMEFARIKI muda mfupi tu baada ya kuwasili Lagos Nigeria akitokea Marekani Daktari kutoka Marekani

Reddington Hospital amethibitisha kifo cha Goldie na kusema chanzo cha kifo chake ni kuziba kwa mishipa wa damu  (atery ya mapafu) ambayo imesababishwa na kuganda kwa damu katika mshipa wa damu kwa lugha ya kitaalamu Coronary Artery ambapo kwa lugha ya kiatalaamu unaitwa Pulmonar embolism.

Mpenzi wake Goldie ambae ni Msanii wa Kenya CMB Prezzo ametua Nigeria usiku huu muda mfupi uliopita kwa ajili ya kuendeleza mipango aliyokua nayo na Goldie ikiwemo kutengeneza show ya TV.
                                
Prezzo alitakiwa kushiriki katika TV show ambayo yeye na Goldie wangekua moja ya wahusika wakuu ambapo mpango ulikua baada ya mwezi mmoja Goldie na Prezzo wangekuja Tanzania, Uganda na Kenya kwa ajili ya kujitangaza na kuipromote single mpya ya Goldie ya ‘Skibobo’ aliyofanya na Ay.


             REST IN PEACE  GOLDIE 

Post a Comment

 
Top