Ni mwanamziki anayekuja vizuri kwenye Tansia ya muziki wetu wa bongo fleva ambapo mpaka sasa amechi single kadhaa ikiwa ni pamoja na ile ya Mziki mtamu ila dada huyu ana mengi ya kusema sasa msikilize hapa..




Ninachojua penye nia pana njia na ukikazana mafanikio yanakuja kwa wakati wake, nikiwa naendelea kuandika mashairi ya nyimbo zangu bado napanga mbinu nyingi za kukabiliana na mziki wa bongo, mwanzo nilipo anza rasmi kurecod haikuwa ngumu sana kwangu coz nilipokelewa vizuri kila studio niliofika na wamekuwa wakionesha mchango mkubwa kwangu kwa vitu vingi,.Kunakitu kina weza kukutokea katika maisha na ukakiwasilisha kwa jamii kwa njia ya muziki, mara nyingi napenda kuimba maisha yetu ya kawaida na mambo mengine ninayokumbana nayo nikiwa kama msichana.





Natarajia kuachia nyimbo yangu karibuni na pia ntashukuru mungu endapo watanzania watanielewa na kunipokea kwani muziki bila mashabiki hakuna chochote waweza fanya, Japo muonekano wangu wengi wananishauri nifanye mitindo lakini mahisi sipo tayari kwa sasa japo napenda sana na naweza vitu vingi vinavohusu mitindo ila daima najua kila jambo linawakati wake . kwa mipango ya mungu nikija kufanikiwa kwenye muziki nina mpango wa kufungua kampuni yangu ya mitindo kwani ninauwezo wa kuchora nguo na kushona pia kudizaini vitu vingi vinavohusu urembo, Najua kwa kufanikisha hili nitaweza kuitangaza nchi yangu vizuri sana kitaifa na kimataaifa kupitia muziki na mitindo







Pamoja na kujua kuimba bado ninauwezo mkubwa wa kudance aina nyingi za muziki wa mataifa mbalimbali pia nimejifunza mengi kuhusu dancing maana nategemea itanisaidia sana katika muziki wangu.

Pia kaa tayari kwa ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la PENZI LAKE 




Post a Comment

 
Top