Baada ya stori nyigi kumwagika na mapicha kibao ya Staa Vanessa Mdee na Jux kuwa na mahasiono lakin baada ya kufanyiwa mahojiano walikataa katakataa na wakasema ni marifiki sasa leo ubuyu umwemwagika




Pichani hapo juu ni Jux akiwa na Vanessa ukiangalia picha unaweza kuwa na majibu mengi sana kutoka na pozi la kimahaba baina yao lakini majibu yote yatakuwa yanaelekea kwenye jibu moja kwamba ni wapenzi 

Kupitia Instagram mapema leo Vanessa Mdee ameposti picha hiyo hapo juu na kuandika maneno hayo hapa chini 


“A1 since Day 1,” 



Mtandao wa Bongo5 uliwahikufanya interview na Vanessa Mdee na alikuwa na haya ya kusema 

‘Nitasubiri’, Vanessa aliwahi kujibu,”Unajua labda watu hawafahamu tu lakini mie na Jux tumefahamiana muda sana na ni mtu ambaye huwa tunashauriana hasa mambo ya kazi zetu.”

“Ni rafiki yangu wa muda sana sasa hivi. Unajua watu wakikuona upo na mtu karibu tu lazima watasema. Mwanzo walisema Ommy Dimpoz sababu ya ile nyimbo ya Me and You. Mara wakasema Gosby kipindi kile ilipotoka ile nyimbo ya Monefere. Kwahiyo kwahiyo hata leo mfano Nahareel asingekuwa na Aika basi nahisi na yeye pia wangesema hivyo. Ila sio hivyo wanavyofikiria. Jux ni rafiki yangu tu,”

Haikuishia hapo naye  Jux alikuwa na haya ya kusema 

 “No ni mshikhaji wangu tu, tunafanya naye kazi, kuna tabia zinaendana, kama ninavyokuwa na rafiki na Stamina, Mo Music ni kawaida, sema unajua ni mwanamke na ni njia toafuti ndio maana imekuwa hivyo, Ni msichana mzuri, mwonekano wake mzuri, she is smart, yeah she is a wife material, yuko vizuri, lakini na mimi tumeendana sana tabia zetu kama washikaji. Sema nipo naye karibu na kwa sababu mimi sionekanagi na wasichana wengi ndio maana imekuwa hivyo. Lakini sijui labda baadaye kwa sasa hivi ni mapema, vyote anapanga Mungu,” 


Mwenye macho haambiwa Tazama ubuyu ulishamwagika hivyo kila la Kheri couple mpya mjini Jux na Vee Money 


Credit Bongo5

Post a Comment

 
Top