Muigizaji wa filamu, Wastara Juma amewapa watu simamzi zito mtandaoni, baada ya leo kuandika maneno mazito ya uchungu akisema matatizo ya dunia yamemzidia na kubandika picha akiwa analia.Na hivyo kupelekea mashabiki wengi kumpa pole na kumtia moyo kuwa yote yana mwisho wake na Mungu ndio mpagaji wa yote.






“Hapa duniani kila mtu ana shida na matatizo lakini kwangu mimi yamezidi daaah eeeh Mungu nibadilishe basi hiyo nafasi ya mteso uliyoniweka muweke mwingine nami unipe furaha nicheke kama wengine maishani mwangu niache kulia eeeh Mungu baba jamani mimii mimiii aah”.-Wastara aliandika baada ya kuweka picha hiyo hapo juu.

Hakuweka wazi nini hasa kimempata,lakini picha hii inaonekana imetoka kwenye moja ya kipande cha filamu

Credit Jamii Forums

Post a Comment

 
Top