Shilole amedai kuwa mpango wake ni kumzalia mchumba wake Nuh Mziwanda watoto wawili.

Muimbaji huyo mwenye watoto wawili wa kike alisema hayo wakati akiongea kwenye kipindi cha The Mboni Show.
 
“Nitamzalia watoto wawili, nina wawili,” alisema Shilole aliyeongezana na mchumba wake huyo kwenye kipindi hicho kinachorushwa TBC1.
 


Shilole alisema kuwa kadri siku zivyonaenda anazidi kumpenda zaidi Nuh kutokana na mapenzi anayomwonyesha. 
 
Mwaka jana Nuh alimvisha pete mchumba wake huyo.

Post a Comment

 
Top