KALOLI Dawa ambaye ni mume wa mtu, amedaiwa kujipiga picha za utupu akiwa na mchepuko wake uliofahamika kwa jina moja la Irene kisha kusambaa mitandaoni.Picha za wawili hao wenyeji wa Wilaya ya Lamadi, mkoani Simiyu zimedaiwa kuvuja mara baada ya rafiki wa Irene kuziiba kwenye ‘laptop’ ya Kaloli na kuzisambaza mtandaoni.

mume wa mtu huyo akiwa na mchepuko.

Imedaiwa kuwa rafiki wa Irene ambaye jina lake halikupatikana mara moja, alizivujisha picha hizo baada ya kugombana na Irene.Imeelezwa kuwa, vijana hao ni watoto wa wafanyabiashara wakubwa hivyo kitendo cha kusambaa picha hizo kimewasononesha.

Mwanahabari wetu aliwatafuta wahusika hao kwa njia ya simu. Irene simu yake haikuwa hewani lakini Kaloli alipatikana na kufunguka:Mwandishi: Habari? Unazungumza na mwandishi wa Global Publishers, nazungumza na Kaloli?
Kaloli: Ndiyo mimi.

Mwandishi: Tunazo picha zako hapo ukiwa uchi wewe na mpenzi wako Irene.
Kaloli: Mmezipataje hizo picha? Mwandishi: Picha zimetapakaa kwenye mitandao ya kijamii.
Kaloli: ‘Plizi’ naomba usitoe hiyo habari.

Mwanahabari wetu alikwenda mbali zaidi kwa kumtafuta mzazi wa Kaloli, Mzee Kaloli kumsikia anazungumziaje tukio hilo.“Ni kweli nimeziona hizo picha yaani ni aibu sana kwangu maana mimi ni mtu na heshima zangu na nimeshamkanya mara kadhaa mwanangu aachane na huyo Irene lakini hata hasikii.

“Asiyesikia la wazazi atafunzwa na ulimwengu nimeshaongea sana na Kaloli atulie na mkewe na hata huyo Irene mbona king’ang’anizi hivyo wakati mwanangu ana mke wake tena ana mtoto mdogo?  Wataniua kabla ya umri wangu nimechoka na tabia za Kaloli ananitia aibu,” alisema Mzee Kaloli.

GPL

Post a Comment

 
Top